Posts

Showing posts from July, 2020

MHE. STANSLAUS MABULA ATETEA UBUNGE JIMBO LA NYAMAGANA

Image
MHE. STANSLAUS MABULA ATETEA UBUNGE KURA ZA MAONI JIMBO LA NYAMAGANA* Mhe. Stanslaus Mabula aongoza kura za maoni  mkutano mkuu wa Jimbo katika mchakato wa awali wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Nyamagana kutafuta mwakilishi atakaye peperusha Bendera Uchaguzi mkuu Octoba 2020.  Mhe. Mabula Mbunge anayemaliza muda wake Katika kipindi Cha 2015-2020 amefanikiwa kuongoza Kura za Maoni  kwa kupata kura 319, akifuatiwa na John Nzwalile aliyepata kura 54 pamoja na John Nzilanyingi aliyepata Kura 46. Mchakato huo umehusisha wanachama 105 waliojitokeza kwenye kinyang'anilo hicho na kupigiwa kura takribani na  wajumbe wa mkutano huo 606. Imetolewa na Ofisi ya Mbunge Jimbo la Nyamagana🇹🇿

SAID KUBENEA AHAMIA ACT WAZALENDO MAPEMA LEO

Image
Hayaaaa hayaaaa sasa nilisema jamani  nilisemaaa Mimi Leo ACT WAZALENDO mambo ni 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥 Kila kukicha tunapokea wanachama tena wenye uwezoo na ushawishi ktk jamii zaoo aisee Karibu UZALENDONI ndugu KUBENEA hakika umechagua chagua sahihi karibu ktk familia ya WAHANGA wenzakoo aiseee mambo ni 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥 Nilisha sema  Mimi sitaki kusema sana lakini ACT WAZALENDO inafanya kila kukicha nisemee aisee mambo ni 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥 Ccm mjiandaee kisaikolojia mwaka huu ndio mwaka wenu wa mwisho hivyoo muanzee kuchukua kila kilicho chenu nawaambieni Nilipoo sema ngoja MVUA INYESHE TUONE PANAPO VUJA hamkunielewaa sasa nazani mtanielewaaa kuwa mpaka sasa kuna pahala panavujaaa hayaa Mimi sisemii tena aiseee ACT WAZALENDO TUPO VIZURI TUMEJIPANGA VYAKUTOSHA KULINDA KURA ZETU NA USHINDI WETU MTAELEWAAAA TUU ACT WAZALENDO TUNASEMAA INAFUUUUUUUUUUUUUUUUUU TUKUTANE 25/10/2020 TUU HUU NI UCHAGUZI WA KUFA NA KUPONA LIWALO ...

MH. HASHIM RUNGWE NA UBWABWA MASHULENI, SERA YA KITAALAMU KWENYE UCHAGUZI 2020

Image
                     JICHO LA KITAALAMU : HASHIMU RUNGWE NA SERA YA UBWABWA MASHULENI. Naandika Magoda Jr . Kitaalamu sera ya Hashimu Rungwe ya ubwabwa wa moto mashuleni ni moja ya sera bora zaidi kwa mustakabali wa taifa letu na inaendana na hadhi ya taifa la uchumi wa kati  wa Tanzania , hakika amefikiria kwa kuweka utaifa mbele kuliko maslahi ya wachache na watanzania wote inabidi tumuunge mkono. 📕 Kitaalamu Hashim Rungwe ametumia lugha ya kisiasa ili kupata umakini wa watu wengi ndio maana katumia neno ubwabwa lakini hoja yake kubwa ni kuhakikisha wanafunzi wetu wanapata chakula bora mashuleni kuanzia chekechea kidato cha sita kwa faida ya mwili na ubongo pia. 📕Duniani kote tafiti zinathibitisha pasi na shaka kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja katika ya chakula bora na ujifunzaji mzuri mashuleni ,lakini pia katika uga wa utatibu wanathibitisha umuhimu wa lishe bora na ukuaji mzuri wa mwili na afya ya akili n...

TANGAZO MAALUM KWA WALIOPATA NAFASI YA KUCHAGULIWA KUJIUNGA JKT KWA MWAKA 2020 FORM SIX

Image
                          Tangazo maalum kwa waliopata nafasi ya kuchaguliwa kujiunga JKT kwa mwaka 2020. Kwa vijana wa kidato cha sita. 

PAUL MAKONDA: FANANI ALIYEIMUDU VYEMA HADHIRA YAKE

Image
*PAUL MAKONDA:FANANI ALIYEIMUDU VYEMA HADHIRA YAKE* Naandika Magoda Jr. Moja kati ya sifa bilioni tatu za fanani basi ni kuitambua na kuimudu vyema hadhira yake bila muachano mkubwa , wale ambao walibahatika kuusoma uga wa fasihi wanaweza kuwa mashahidi katika hilo. Pual Makonda au unaweza muita Baba ake na Keegan Kwa nafasi yake aliweza vyema kuendana na mirindimo ya wanadaresalamu na dar es alamu yenyewe na mpaka kijiti kinakabidhiwa kwa mwingine ile hadhi ya jiji la Dar es salaam ilikuwa bado iko juu kileleni. Paul Makonda namuona kama fanani aliyeimudu vyema hadhira yake kwa sababu aliweza fika kujipambanua kulingana na makundi mengi ya wanadaresalamu  na alifanikiwa katika hilo maana mkoa wa Dar es salaam sio wa mchezo mchezo .  Paul Makonda kijiti chake kimepata mtu mwingine lakini wanadaresalamu na Dar es salaam mchango wake utaendelea kukumbukwa sana na jina lake litabaki mioyoni mwa wanadaresalamu kutoka makundi mbalimbali ya wananchi wa jiji la Dar es...

JOTO LA UCHAGUZI TANZANIA 2020 MEMBE AJIUNGA ACT WAZALENDO RASMI

Image
.Ni wiki ya HEKAHEKA, Juma la Kukuru kukara, Nina maanisha nini? Twende na Engias Engima aka mtoto wa mwanamke. Ni kuhusu watia nia ya ubunge kua watia mia. Ni kwa nini? Tumeshuhudia watu wengi waliochukuliwa na MAFURIKO 2015,waliorudishwa na UPEPO,si wa kisulisuli Upepo wa jitahida za serikali safi na nzuri iliojipambanua kufanya vyema 2016-2020. Wengi wa hawa watia mia,kwamba ni mamia wamegawanyika kwenye makundi yafuatayo: 1:Wakufunzi, professors na PhD,hawa wanahitaji wainuliwe toka mavumbini waketishwe na wafalme,wamechoka kufundisha na kutoa Course  work(ya kuwakata watu alama na kulazimisha wahongwe,hawa ninawahabarisha kwamba wawe tayari kuambulia,kura sifuri hadi tano kama alama za darasani. 2;Watumishi wa uma ambao wamechungulia fursa za teuzi inatokana na wenzao waliowahi kugombea na wakaulamba UDAS,Ukurugenzi,nk miongoni mwa hawa wapo walimu waliochoka na chaki,madaktari waliochoka kututibu,nk 3: Watumishi wa dini mfano wachungaji,maaskofu,mapadre,mashehe,wag...

MAAJABU YA DUNIA MWIZI AMSAIDIA MTOTO

Dereva mwizi aligundua kuwa mtoto alikuwa amelazwa katika kiti cha nyuma. Picha: Hisani Mwizi huyo ambaye alikuwa na nia ya kuliaba gari hilo mara moja baada ya kugundua kuwa wawili hao wamezama dukani, aliitumia ujuzi wake na kuingia kwenye gari hilo na moja kwa moja akaanza kuendesha upesi . Baada ya kuenda kwa muda, dereva mwizi aligundua kuwa mtoto alikuwa amelazwa katika kiti cha nyuma baada ya mtoto huyu kuanza kulia kwa hasira. Jamaa huyo alichanganyikiwa kuhusu la kufanya, kwa njia isiyo ya kawaida, jamaa huyo alilazimika kulirejesha gari hilo hadi alikolichukua baada ya kushindwa kuhimili kelele ya mtoto. Alipowasili, aliegesha gari na kuchukua mtoto huyo hadi ndani ya duka hilo kuwatafuta wazazi wake. Aliwaambia kuwa walisahau kufunga mlango wa gari lao na kuwa mtoto wao alikuwa akilia na ndipo akaamua kumsaidia. Wanandoa hao walimpongeza pakubwa kwa kumuokoa mwanao pasi kujua kuwa huyo alikuwa mwizi na kuwa mwano ndiye aliyeliokoa gari lao. Maajabu hayaishi.

UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO, DALILI NA TIBA ZAKE

Zipo aina kuu mbili za vidonda vya tumbo; vinavyotokea ndani ya mfuko wa tumbo, yaani ‘gastric ulcers’, pili hutokea kwenye sehemu ya mwanzoni ya utumbo mwembamba inaitwa ‘duodenal ulcers’. CHANZO CHAKE Katika utumbo, huwa unamwagwa tindikali kwa ajili ya kusaidia mmeng’enyo wa chakula. Kwa kawaida, tindikali huwa ni kali na isipodhibitiwa tumboni, inaweza kuleta madhara. Mfuko wa tumbo wa binadamu una ukuta wa ndani, uliozungukwa na ute (mucus) unaosaidia kuzuia tindikali isiunguze au kuharibu sehemu hiyo. Uzalishaji ute huo unapopungua, una kawaida ya kusababisha tindikali ama kuunguza/kuharibu sehemu ya ukuta wa tumbo, hivyo kusababisha vidonda vya tumbo. Kupungua ute husababishwa na mambo. Kuna maambukizi ya bakteria ajulikanaye kwa jina la ‘helicobacter pylori’ (H. pylori), matumizi ya kipindi kirefu ya dawa za kundi la ‘Nsaids’ kama vile aspirini na ‘ibuprofen.' Pia, mazingira ya kuwepo tindikali nyingi iliyopitiliza tumboni (hyperacidity) ni hali inayohusiana na ...

KIFUNGO KWA KUCHAPISHA HABARI ZA UONGO KUHUSU COVID19

Mwana blogu nchini Tunisia amehukumiwa kifungo cha miezi sita gerezani baada ya kuchapisha taarifa kuhusu Covid-19 ikiwa imeandikwa kwa mtindo wa aya kutoka kwenye kitabu kitakatifu cha Koran. Emna Charqui,28, alikamatwa mwezi Mei kwa kuchapisha ujumbe kwenye ukurasa wa Facebook akiwataka watu kufuata sheria za usafi kwa kuigiza namna ambavyo kitabu hicho kitakatifu kinaeleza. Charqui alisema kwenye mahojiano ya hivi karibuni kuwa hakuwa na nia ya kusababisha taharuki, lakini aliona kuwa ujumbe huo unafurahisha. Alikutwa na hatia katika mahakama ya mjini Tunis kwa kosa la ”kuchochea chuki miongoni mwa watu wa dini tofauti.” Charqui ana mpango wa kukata rufaa. Tarehe 2 mwezi Mei, Charqui aliweka kwenye mtandao wa kijamii ujumbe akiigiza aya kutoka kwenye Koran. Kwenye maandishi aliwataka watu kunawa mikono na kuzingatia kutotangamana ili kudhibiti janga la virusi vya corona. Picha aliyoiweka kwenye ujumbe wake imeripotiwa kubuniwa na kuwekwa mitandaoni na mtu mmoja raia wa A...

Adense

<script data-ad-client="ca-pub-7506385744230213" async src="https://pagead2.googlesyndication.com/pagead/js/adsbygoogle.js"></script>